Kenya na Tanzania zamwokoa Prezzo

 

Tanzania na Kenya ni nchi pekee zilizomwokoa Prezzo na panga la eviction jana. 

Kenya ambako ndiko Prezzo anatokea, imempigia kura zaidi mtu wao ili kuendelea kumwekea uhakika wa kubaki kwenye jumba la Big Brother Africa na hatimaye kujihakikishia kurudi nyumbani na kitita cha dola laki 3.

 

Kama historia inavyosema kwamba mama yake Prezzo ni mtanzania, basi hilo linajidhihirisha kwa watanzania kuwa mstari wa mbele kumpigia kura pia.

Urafiki alionao na wasanii wengine wa Tanzania hususan Ay na MwanaFa umemsaidia kwakuwa wasanii hao wamekuwa mstari wa mbele kuwasisitiza watanzania kumpigia kura Prezzo.

 

"Kenya really appreciates the effort and help you and your fellow country peeps put in voting for Prezzo to stay in the BBA house," ni tweet ya wakenya iliyoelekezwa leo na wakenya.

Jana mshiriki mwingine kutoka Kenya, Malonza na Junia kutoka Namibia waliyaaga mashindano hayo.

Hivi ndivyo Afrika ilivyopiga kura na kuamua matokeo ya jana.

Angola: Junia

Botswana: Lady May

Ghana: Goldie

Kenya: Prezzo

Liberia: *Goldie / Lady May

Malawi: Kyle

Namibia: Lady May

Nigeria: Goldie

South Africa: Lady May

Sierra Leone: Lady May

Tanzania: Prezzo

Uganda: Kyle

Zambia: Malonza

Zimbabwe: Lady May