Tyrese, Ginuwine, na Tank waunda kundi, wamponda Usher na wengine kwa kuiharibu R&B

Muimbaji na muigizaji Tyrese Gibson ameonekana kuwarushia madongo wasanii wenzake akiwemo Usher na Chris Brown walioperform kwenye tuzo za BET kwa namna walivyoubadilisha muziki wa  R&B.

Usher alitumbuiza kwa wimbo wa 'Climax' kwenye tuzo hizo zilizofanyika alfajiri ya leo kwa saa za Afrika Mashariki, wimbo uliopo kwenye albam yake ya Looking 4 Myself.

 

Hata hivyo mtu mmoja ambaye hajapendezwa na performance hiyo iliyosifiwa na wengine kutokana na uimbaji mpya wa Usher, ni Tyrese,anayedai kuwa  R&B ya ukweli ipo kwenye kundi lake linaloundwa  na yeye, Tank na Ginuwine.

"Hatuna house, hatuna techno...tunakuja na  R&B ya ukweli," Tyrese aliandika kwenye Twitter.

“R&B imeharibiwa. Tunakuja kuwakumbusha nyote kwanini mlipenda muziki wa RNB. TGT inakuja siku si nyingi."