Wema Sepetu ashangazwa na wingi wa email anazopata baada ya kuanzisha kampuni na kutangaza ajira

Hivi karibuni Miss Tanzania wa zamani, Wema Sepetu alizindua rasmi ofisi za kampuni yake iitwayo Endless Fame Films zilizopo maeneo ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam. Uzuri wa ofisi zake unadaiwa kuifanya kampuni yake kuwa ya kwanza nchini ya aina hiyo yenye ofisi za nguvu zaidi. Baada ya kutangaza nafasi za kazi mbalimbali wiki hii, Wema ameshangazwa na wingi wa email alizopokea kiasi cha kupost picha kwenye Instagram yenye maneno: da emails omg... im tryng ma best to reply ol of dem....